Home » » ZANZIBAR KUIMARISHA KANUNI ZA KUKATAZA MATUMIZI YA TUMBAKU KATIKA KULINDA AFYA ZA WANANCHI

ZANZIBAR KUIMARISHA KANUNI ZA KUKATAZA MATUMIZI YA TUMBAKU KATIKA KULINDA AFYA ZA WANANCHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Zanzibar Dkt Ghirmay Andemichael akitoa maelezo ya Shirika hilo kwenye warsha ya siku tatu ya kuimarisha kanuni za kupambana na matumizi ya tumbaku inayofanyika Hoteli ya Golden Tulip Malindi Mjini Zanzibar.
 Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Jamala Adam Taib akifungua warsha ya kuimarisha kanuni za mapambano ya matumizi ya bidhaa zinazotokana na tumbaku katika Hoteli ya Golden Tulip Malindi Mjini Zanzibar.
 Dkt. William Maina kutoka WHOAFRO akitoa maelezo ya Azimio la WHO na sheria za kimataifa dhidi ya mapambano ya matumizi ya bidhaa zinazotokana na tumbaku katika warsha ya kuimarisha kanuni za mapambano hayo katika Hoteli ya Golden Tulip Malindi.
 Baadhi ya washiriki wa warsha ya kumiarisha mikakati ya kanuni za kupiga vita matumizi ya tumbaku inayofanyika Hoteli ya GoldenTulip Malindi Mjini Zanzibar.

Picha ya pamoja ya mgeni rasmi na washiriki wa warsha ya kuimarisha mikakati ya kupiga vita matumizi ya tumbaku inayofanyika Hoteli ya Goden Tulip Malindi Mjini Zanzibar.Picha na Makame Mshenga.

Na Ramadhani Ali - Maelezo.

Wizara ya Afya Zanzibar inaendelea kuimarisha kanuni za kupunguza matumizi ya tumbaku baada ya kuundwa sheria ya Afya ya Jamii ya mwaka 2012 na kuridhia Azimio la Shirika la Afya ulimwenguni (WHO) kupiga vita bidhaa zinazotokana na tumbaku katika kunusuru afya za wananchi.

Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Jamala Adam Taib amesema Wizara hiyo tayari imeweka kanuni ya kukataza kuvuta sigara kwenye mikusanyiko ya watu katika kuwanusuru waathirika wa moshi wa sigara bila ya kuwa wavutaji.

Dkt. Jamala ameeleza hayo alipokuwa akifungua warsha ya siku tatu ya kuimarisha kanuni za kupambana na matumizi ya tumbaku katika Hoteli ya Golden Tulip iliyopo Malindi iliyowashirikisha wadau kutoka taasisi mbali mbali za Serikali.

Mkurugenzi Mkuu alisema uvutaji wa sigara umeonekana kuwa chanzo kikubwa cha ongezeko la maradhi yasiyoambukiza ikiwemo saratani, sukari maradhi ya mapafu na maradhi ya ini.Alisema pamoja na kwamba Zanzibar haizalishi tumbaku na haina viwanda vinavyohusika na bidhaa za tumbaku bado wananchi wamekuwa waathirika wa moshi wa sigara.

Alieleza kuwa tafiti zilizofanyika zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watu wanaofariki kutokana na maradhi hayo yanatokana na kuvuta sigara ambapo asilimia 15 ya vifo hivyo vinawafika watu wanaovutishwa moshi na wavutaji wa sigara bila ya wao kushiriki kuvuta.

Katika kufanikisha lengo  hilo Dkt. Jamala alizishauri taasisi za Serikali, Jumuiya za kiraia na jamii kwa jumla kuunga mkono kanuni inayokataza sigara kuvutwa kwenye mikusanyiko ya watu  na nyengine zinazoundwa ili kulinda afya zao.

Mwakilishi wa WHO Zanzibar Dkt. Ghirmay Andemichael alisema Zaidi ya watu milioni saba wanapoteza maisha kila mwaka duniani kutokana na matumizi ya bidhaa zinazotokana na tumbaku ambapo asilimia 80 ya vifo vinatokea katika mataifa yanayoendelea.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa