Home » » KAMISHENI YA KUKABILIANA NA MAAFA ZANZIBAR YAVUTIWA NA URATIBU WA AFYA MOJA TANZANIA BARA

KAMISHENI YA KUKABILIANA NA MAAFA ZANZIBAR YAVUTIWA NA URATIBU WA AFYA MOJA TANZANIA BARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 Mratibu maafa Ofisi ya Waziri Mkuu , Edgar Senga akiwasilisha mada ya majukumu ya idara hiyo wakati wa kikao cha kubadilishana uzoefu na  Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa ya Zanzibar walipofanya ziara ofisini hapo leo tarehe 15 Novemba, 2017,jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Operesheni na Huduma za Binadamu Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa  Zanzibar, Makame Khatib akiwasilisha mada ya majukumu ya Kamisheni hiyo wakati wa kikao cha kubadilishana uzoefu na  Idara ya Kuratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, walipofanya ziara ofisini hapo leo tarehe 15 Novemba, 2017,jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi  Msaidizi Idara ya Kuratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Bashiru Taratibu akifafanua jambo wakati wa kikao cha kubadilishana uzoefu na  Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa ya Zanzibar walipofanya ziara ofisini hapo leo tarehe 15 Novemba, 2017,jijini Dar es Salaam, wengine ni waratibu wa maafa kutoka Zanzibar na Tanzania Bara.


Kamisheni ya Kukabiliana na maafa Zanzibar imevutiwa na shughuli za kuratibu maafa nchini zinazofanywa na serikali ya awam ya Tano kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu,Idara ya Kuratibu maafa ikiwa ni pamoja na kuratibu Afya moja ambapo katika Dhana ya Afya Moja, sekta ya   afya ya binadamu, wanyama (pori na wafugwao) na mazingira, zinakuwa na mawasiliano ya karibu kiutendaji na kupanga  mikakati ya pamoja katika kujiandaa na milipuko ya magonjwa na kukabiliana nayo endapo itatokea.

Akiongea wakati wa  ziara ya Kubadilishana Uzoefu na Idara ya Kuratibu Maafa na Ofisi ya Waziri Mkuu,jijini Dar es salaam leo tarehe 15 Novemba 2017, Mkurugenzi Mtendaji Kamishseni ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar, Shaban Mohamedi amebainisha kuwa kamisheni yake imevutiwa na jinsi idara ya maafa inavyoweza  kuimarisha juhudi na ushirikiano wa sekta mbalimbali katika maandalizi ya kuzuia,kujiandaa na kukabili  magonjwa ambukizi kwa kujumuisha sekta zote muhimu.

“Tutaupitia mpango mkakati wa Afya moja  ili nasisi tuanze juhudi za kuratibu Afya moja  kwani  Kamisheni inajukumu lakukabiliana na Maafa hivyo tutachukua juhudi za kuhakikisha na sisi Zanzibar tunashirikiana na wadau husika ili tuweze kutumia rasilimali ndogotulizonazo kuweza kukabili  magonjwa yatokayo kwa  wanyama kwenda kwa binadamu yanayoiathiri jamii ya Zanzibar” alisisitiza Khatibu

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa