Home » » MFUMO WA RAIS WA KUKUSANYA MAPATO KIELEKTRONIKI UMEPEISHA MAPATO YA KODI YA MAKAMPUNI YA SIMU KWA 102%

MFUMO WA RAIS WA KUKUSANYA MAPATO KIELEKTRONIKI UMEPEISHA MAPATO YA KODI YA MAKAMPUNI YA SIMU KWA 102%

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na Mwandishi wetu. Mfumo wa Kukusanya Mapato Kielekroniki (eRCS) umeonyesha mafanikio makubwa kwa miezi mitatu ya mwanzo ya Julai, Agosti na Septemba 2017, baada ya Makusanyo ya Kodi kwa Upande wa Zanzibar (ZRB) kupitia eRCS kufikia Shilingi Bilioni.7.2, ukilinganisha na Shilingi Bilioni 3.5, ZRB walizokusanya kipindi Kama hicho mwaka 2016 kabla ya mfumo wa eRCS. Makusanyo hayo yakiwa ni Ongezeko la Shilingi Bilioni 3.6 sawasawa na asilimia102%. Ni zaidi ya Mara mbili ya makusanyo ya mwaka Jana kabla ya mfumo wa eRCS, yanayofikia shilingi Bilioni 7.2 ni majumuisho wa Ushuru wa Bidhaa (Excise Duty) na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) Baada ya kukata Marejesho.
Wakati huo huo Taarifa tulizonazo kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni kwamba makusanyo ya kodi yanayotokana na kampuni za simu, kwa kutumia eRCS TRA wamefanikiwa kuongeza makusanyo kwa asilimia 21% kwa kukusanya Jumla ya shilingi Bilioni 128.9 kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai, Agosti na Septemba 2017, ukilinganisha na makusanyo ya miezi ya Aprili, Mei na Juni 2017 kabla ya kuanza kutumia mfumo wa eRCS. Aprili, Mei na Juni 2017 kabla ya eRCS, makampuni ya simu saba yalilipa jumla ya kodi ya Shilingi Bilioni 101.7. Julai, Augusti na Septemba 2017, baada ya kuanza kutumika eRCS, Makampuni ya simu yale yale yameweza kulipa Shilingi Bilioni 128.9. Kukiwa na ongezeko la Shilingi Bilioni 27.2 sawa na 21% ambazo ni majumuisho yaliyotokana na kodi ya Ongezeko la thamani (VAT) na Ushuru wa Bidhaa (Excise Duty).
Ukijumuisha makusanyo yanayotokana na Kodi kutoka kampuni za simu saba kuanzia mwezi Aprili 2017 mapaka mwezi Septemba 2017 TRA imekusanya Jumla ya Shilingi Bilioni 230.7. kwa kipindi cha miezi sita tu, ambazo ni wastani wa shilingi Bilioni 38.5 kwa mwezi. Taarifa tulizopata kutoka chanzo chetu ambao hawakutaka majina yao yatajwe wametueleza kwamba Serikali inafuatilia kwa kina udanganyifu unaofanywa na kampuni za simu katika Taarifa zao walizozipeleka TRA za input kwa ajili ya “return” ambazo zinakosa uhalisia kwani zinajumuisha taarifa za miezi iliyopita kwa lengo la kuongeza kiwango cha input tax.
Mfumo eRCS ulizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar Dkt. Mohamad Shein walipozindua Dirisha la kukusanya kodi Kielekroniki Elecrtronic Revenue Collection System (eRCS) tarehe 1 Juni 2017, ukiwa na lengo la kusaidia Mamlaka zote mbili za Mapato yaani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRB) kuongeza mapato yanafanyika kupitia njia za kielektroniki. Mpaka Mwezi Novemba 2017, ni kampuni saba za simu ndizo zilizounganishwa katika mfumo wa eRCS, Kampuni hizo ni Vodacom, TTCL, Airtel, tiGO, Halotel, Zantel na Smart. Taarifa hii imeandikwa kutokana na taarifa zinazopatikana IDC, TRA na ZRB Novemba 2017

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa