NSSF YAIPONGEZA ZANZIBAR HEROES KWA USHINDI WA KOMBE LA MAPINDUZI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, amepokea kiasi cha shilingi milioni 10 kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kama pongezi kwa ushindi wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes). Timu hiyo ilishinda kwa magoli 2-1 dhidi ya Timu ya Taifa ya Burkina Faso katika mchezo wa fainali wa Kombe la Mapinduzi uliofanyika tarehe 13 Januari 2025, kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba.Hundi hiyo ilikabidhiwa kwa Mhe. Rais na Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF, Bi. Lulu Mengele, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba. Kulia kwa Mhe. Rais ni Mhe. Mama Mariam Mwinyi, na kushoto kwake...

WATU WANAOSADIKIKA KUWA NI ASKARI JAMII WATUHUMIWA KUMPIGA MWANAMKE ZANZIBAR

Na Nihifadhi Abdulla, ZanzibarWATU wanaosadikika ni askari jamii wamedaiwa kumpiga Mwanamke na kumsababishia majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake.Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Bwejuu Wilaya ya kusini Mkoa wa kusini Unguja mhanga wa tukio hilo (jina limehifadhiwa) amesema tukio hilo limetokea mnamo Desemba 24, 2024 siku ya mkesha wa kumbukizi za sikukuu za kuzaliwa bwana Yesu Kristu Krismasi."Mimi nilikua natoka kwenye sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yangu apo kwa LILA ndio akatokea huyo mwanamme akanipeleka Kwa wenzake na kuanza kunipiga Kwa kutumia waya wa umeme"Amesema baada ya tukio hilo Kwa msaada wa wasamaria wema amefika...

RAIS MWINYI:SERIKALI INAJIPANGA UJENZI WA MAGHALA YA CHAKULA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuwa Serikali inajipanga kwa Ujenzi wa Maghala ya Kuhifadhia Chakula ili kuwa na Uhakika wa Chakula hivyo kujitokeza kwa Sekta binafsi kuanza kujenga ghala ni jambo linalopaswa kuungwa Mkono.Rais Dk.Mwinyi ameyasema hayo alipofungua ghala la Kuhifadhia chakula Gando , Wilaya ya Wete ,Mkoa wa Kaskazini Pemba linalomilikiwa na Kampuni ya Yasser Provision .Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali inalenga Kuwapunguzia Mzigo wa Gharama Wafanyabiashara wanaoleta chakula nchini ili kuwepo kwa Unafuu wa bei kwa Wananchi.Rais Dk.Mwinyi ameielezea njia nyengine ni kuwa na...

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR- KUFUNGUA TAMASHA LA UTAMADUNI-MAHONDA - KWA NIABA YA RAIS WA ZANZIBAR

   Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo itaendelea kuweka Mazingira bora ya kuendeleza sanaa na utamaduni wa Mzanzibari nchini kwa maslahi mapana  ya vizazi vya sasa na baadae.   Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt Hussein Mwinyi katika hafla ya ufunguzi wa Tamasha la ishirini na Tisa ( 29 ) la Utamaduni wa Mzanzibari lililofanyika katika  uwanja wa Misuka Mahonda Mkoa wa Kaskazini Unguja. Amesema Serikali tayari imeanza ujenzi wa nyumba ya Sanaa Mwanakwerekwe...

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Kutajenga hospitali ya Mkoa maeneo

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itajenga hospitali kubwa ya Mkoa maeneo ya Mahonda, Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Unguja ambayo itafadhiliwa na Serikali ya Oman.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman anayeshughulikia Utawala na Fedha, Khalid Almuslahi.Dk. Mwinyi amesema ujenzi wa hospitali hiyo ni muhimu kwa dhamira ya Serikali ya kuwa na hospitali kubwa kwa kila Mkoa ili kuwafikishia wananchi huduma bora karibu na makaazi yao na kupunguza msongamano kwenye hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja.Rais Dk. Mwinyi...

POLISI ZANZIBAR YAMDAKA TAPELI KWA KUJIZOLEA MILIONI 6 AKIJIFANYA ANANAFASI YA KAZI YA USALAMA WA TAIFA

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ACP Abubakar Khamis Ally akizungumza na Waandishi wa Habari, Ofisini kwake Madema, Zanzibara. ..........................Polisi, ZanzibarJeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi linamshikilia Marco Daud Zagamba (32) wa Mbweni, kwa tuhuma za kujipatia sh. milioni 6 kwa njia ya utapele wa kuwapatia ajira watu mbalimbali kati Idara ya Usalama wa Taifa na vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Madema, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ACP Abubakar Khamis Ally amesema mtuhumiwa huyo aliwatapeli wananchi kwa kuwaahidi kuwapatia ajira...

Makamu wa Rais ahimiza maadili ili kuvutia jamii kushiriki michezo, mazoezi.

ZANZIBAR.MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Mhe. Othman Massoud Othman amevitaka vikundi vya mazoezi nchini kuweka kanuni na miongozo ya maadili ambayo itasaidia kuondoa mitizamo hasi kwa jamii juu ya ushiriki wa makundi yote katika vikundi vya mazoezi na michezo.Ametoa wito huo wakati akizungumza na vikundi vya mazoezi katika halfa ya kuhamasisha ushiriki wa jinsia zote kwenye mazoezi na michezo ikiwa ni  maadhimisho ya kutimia miaka kumi ya klabu ya mazoezi Gombani kisiwani Pemba.Alisema, kuwepo kwa kanuni zinazosimamia maadili katika mazoezi na michezo kutasaidia watu wengi hasa wanawake kuona eneo hilo ni salama kwao na kuondoa...

RAIS WA ZANZIBAR ALHAJJ DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEJUMUKA NA WANAFAMILIA NA WANANCHI KATIKA MAZIKO YA MAREHEME ZULEKHA AHMED ABDALLAH

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussei Ali Mwinyi  akijumuika na Viongozi wa Serikali, Dini na Wananchi katika maziko ya aliyekuwa Mke wa Marehemu Sheikh.Hyder Jabir Saleh E-Farsy,Marehemu Zulekha Ahmed Abdallah,yaliyofanyika katika viwanja vya Msikiti Mkuu wa Ijumaa Malindi Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar .(Picha na Ikulu).&nb...

RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AZUNGUMZA NA UJUMBE KUTOKA JIMBO LA SHANDONG CHINA IKULU ZANZIBAR.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Mhe.Zhang Xinwen Makamu Mwenyekiti wa (CPPCC) kutoka Jimbo la Shandong Jamhuri ya Watu wa China, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 17-7-2024.(Picha na Ikulu)RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe kutoka Jimbo la Shandong Jamhuri ya Watu wa China, ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa (CPPCC) Mhe.Zhang Xinwen (kulia kwa Rais) akiwa na ujumbe wake,mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 17-7-2024.(Picha...

RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEFUNGUA TAMASHA LA MWAKA KOGWA MAKUNDUCHI MKOA WA KUSINI UNGUJA LEO 16-7-2024

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akipata maelezo ya vyakula vya asili kutoka kwa Mzee wa Makunduchi Bi.Amina Ubwa Ali,baada ya kulifungua Tamasha la Mwaka Kogwa 2024, linalofanyika katika viwanja vya Kae Kuu Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja  16-7-2024.na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud.(Picha na Iku...

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AMEIFUNGUA BUSTANI YA MNAZI MMOJA MJI MKONGWE JIJINI ZANZIBAR LEO

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kuifungua Bustani ya Mnazi Mmoja Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar, iliyoko jirani na Hospitali ya Mnazi Mmoja, ufunguzi huo uliyofanyika leo 15-7-2024, na (kulia kwa Rais) Mwenyekiti wa Kampuni ya Infinity Group Bw. Samuel Saba na ( kushoto kwa Rais) Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga.(Picha na Iku...

RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AMEUFUNGUA MKUTANO WA WAZALISHAJI WA SUKARI WA NCHI ZA SADC UKUMBI WA HOTELI YA GOLDEN TULIP UWANJA WA NDEGE ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kuufungua Mkutano wa Wazalishaji wa Sukari katika Nchi SADC, ufunguzi huo uliyofanyika leo 10-7-2024 katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa TUZO Maalum na Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji Sukari Tanzania (TSPA)Bw.Seif Ali Seif, baada ya kuufungua Mkutano wa Wazalishaji wa Sukari kwa Nchi za SADC, unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja...

DKT. JAFO AAHIDI USHIRIKIANO KWA WAFANYABIASHARA

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo (Mb) ameihakikishia sekta binafsi hususani Wafanyabiashara na Wawekezaji wa Viwanda kuwa watapata ushirikiano mkubwa katika kutatua changamoto mbalimbali za kibiashara ili kuhakikisha wanafanya biashara kwa chini ya uongozi wake.Ameyasema hayo Julai 5, 2024, alipokuwa akizungumza na baadhi ya Taasisi zilizochini ya Wizara yake zinazofanya kazi kwa ushirikano kati ya Tanzania Bara na visiwani zinazohusika na masuala ya biashara mara baada ya hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, Aidha Dkt Jafo ametiwa wito kwa Wizara za Kisekta na sekta binafsi...
 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa