Home » » Hoteli ya Karume kubinafsishwa Zanzibar

Hoteli ya Karume kubinafsishwa Zanzibar

SERIKALI ya Zanzibar imetangaza mpango wake wa kuibinafsisha Hoteli ya Bwawani kwa wawekezaji wenye uwezo wa kuiendesha kibiashara katika mwaka huu wa fedha.
Mpango huo umetangazwa jana mjini Zanzibar na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo, Said Ali Mbarouk, wakati alipokuwa akifunga mjadala wa bajeti yake katika kikao cha Baraza la Wawakilishi.
Hoteli ya Bwawani ilianza kujengwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Aman Karume, kabla ya kuuawa kwa kupigwa risasi na wapinga maendeleo mwaka 1972.
Waziri Mbarouk alisema akipatikana mwekezaji makini atapatiwa kuendesha hoteli hiyo ili ijiendeshe kibiashara na kukuza mapato ya sekta ya utalii Zanzibar.
Alibainisha kuwa mpaka sasa haijafahamika hatima ya wafanyakazi wa Shirika la Utalii Zanzibar (ZTC) wapatao 119 ambalo serikali imeamua kulivunja kuanzia mwaka huu.
Waziri Mbarouk alisema serikali ipo katika hatua za kubinafsisha Hoteli ya Bwawani ambayo sasa inakabiliwa na uchakavu mkubwa na kusababisha sehemu kubwa ya hoteli hiyo kutotumika.
Waziri Mbarouk alisema katika mwaka wa fedha 2012/13 ilikusanya sh milioni 826.9 na ilitumia shilingi 817.9 sawa na asilimia 99 ya makusanyo ya mapato yake.

CHANZO TANZANIA DAIMA

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa