Chama cha Wananchi (CUF) kimeishauri Serikali ya
Jamhuri ya Muungano kuendesha zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu
visiwani Zanzibar kutokana na kuwapo kwa wimbi la wahamiaji hao ili
kuweza kupunguza vitendo vya uhalifu ikiwemo matumizi ya mabaya ya tindikali.
Kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi wa Mawasiliano, Habari na
Haki za Binadamu wa chama hicho, Salum Bimani, jana.
Alisema Tanzania ni nchi mbili zilizoungana hivyo zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linapaswa kuendeshwa nchi nzima na si kwa Tanzania Bara pekee kwani wahamiaji haramu wameenea katika pande zote hususan katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Alisema chama hicho kimeunga mkono zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linaloendelea Tanzania Bara hivyo zoezi hilo kuihusisha na Zanzibar kwani litasaidia kupunguza vitendo vya uhalifu ikiwemo matumizi mabaya ya tindi kali ambayo yameshamiri visiwani Zanzibar.
“Inashangaza kuona zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linafanywa Tanzania Bara peke wakati sisi ni nchi mbili zilizoungana kuunda Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Bimani.
Chama hicho kimetoa agizo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kulifanyia kazi suala hilo ili zoezi hilo lisaidie haki kutendeka kwani tayari kuna fununu kwamba baadhi ya wahamiaji haramu waliopo Zanzibar wameshapatiwa vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi na upo uwezekano wa kupiga kura mwaka 2015 katika uchaguzi mkuu.
Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Hamad Masoud, aliitaka Zanzibar pamoja na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kulifanyia uhakiki daftari la Wapigakura kabla ya uchaguzi mkuu kutokana na alichodai kuwa daftari hilo lina kasoro nyingi ikiwamo watu wasiokuwa na sifa ya kuandikishwa wameandikishwa katika daftari hilo .
Alisema Tanzania ni nchi mbili zilizoungana hivyo zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linapaswa kuendeshwa nchi nzima na si kwa Tanzania Bara pekee kwani wahamiaji haramu wameenea katika pande zote hususan katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Alisema chama hicho kimeunga mkono zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linaloendelea Tanzania Bara hivyo zoezi hilo kuihusisha na Zanzibar kwani litasaidia kupunguza vitendo vya uhalifu ikiwemo matumizi mabaya ya tindi kali ambayo yameshamiri visiwani Zanzibar.
“Inashangaza kuona zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linafanywa Tanzania Bara peke wakati sisi ni nchi mbili zilizoungana kuunda Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Bimani.
Chama hicho kimetoa agizo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kulifanyia kazi suala hilo ili zoezi hilo lisaidie haki kutendeka kwani tayari kuna fununu kwamba baadhi ya wahamiaji haramu waliopo Zanzibar wameshapatiwa vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi na upo uwezekano wa kupiga kura mwaka 2015 katika uchaguzi mkuu.
Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Hamad Masoud, aliitaka Zanzibar pamoja na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kulifanyia uhakiki daftari la Wapigakura kabla ya uchaguzi mkuu kutokana na alichodai kuwa daftari hilo lina kasoro nyingi ikiwamo watu wasiokuwa na sifa ya kuandikishwa wameandikishwa katika daftari hilo .
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment