Home » » RC KASKAZINI PEMBA APONGEZA ACTION AID KWA KUTETEA HAKI ZA WANAWAKE

RC KASKAZINI PEMBA APONGEZA ACTION AID KWA KUTETEA HAKI ZA WANAWAKE


Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Dadi Faki Dadi amelipongeza Shirika la Action Aid kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya umaskini na utetezi wa uvunjivu wa sheria juu ya kulinda haki za wanawake Visiwani Zanzibar.

Katika hotuba iliyosmwa na kwa niaba yake na Afisa Tawala Mkoa huo Mwalim Khamis Salim Mohammed kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukandamizaji wa wanawake , amesema kuwa uwamuzi wa shirika hilo umetoa fursa ya kujenga jamii ya wazanzibar iliyo na uadilifu .

Aidha amefahamisha kwamba Serikali nayo kwa upande wake imechukua hatua kukabiliana na matendo hayo , ambapo miongoni mwa hatua hizo ni kuanzisha vituo vya mkono kwa mkono pamoja na madawati ya wanawake .

Amesema kuwa pamoja na changamoto  mbali mbali zinazojitokeza siku hadi siku , ikiwemo ucheleweshwaji wa kesi mahakamani , rushwa na gharama za kufuatilia kesi lakini hakuzuii wahalifu kushawishika kuachana na vitendo hivyo .

Nao washiriki wa maadhimisho hayo wameshauri elimu ya ukatili wa kijinsia na udhalilishaji wa wanawake  na watoto ianze kutolewa maskulini ili kuwajenga uwelewa watoto wa kike jinsi ya kukabiliana na matendo hayo .

Aidha wameshauri wahusika wanaofanya suluhu baada ya kesi ya udhalilishaji kufikishwa Polisi wachukuliwe hatua ili kukomesha kuwepo na tabia hiyo ndani ya jamii .



0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa