Home » » zanzibar-yang-ara-chalenji-bara-kucheza-leo

zanzibar-yang-ara-chalenji-bara-kucheza-leo

TIMU ya soka ya Taifa ya Zanzibar, ‘Zanzibar Heroes’ jana ilianza vema michuano ya Kombe la Chalenji baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Sudan Kusini.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Nyayo, Nairobi kuanzia saa nane mchana, timu zote zilionekana kushambuliana kwa zamu, lakini Zanzibar ilionekana kutumia uzoefu kuizidi maarifa timu ngeni kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Sudan Kusini.
Zanzibar ilikuwa ya kwanza kupata bao la kuongoza likifungwa na Suleiman Kassim Selembe kabla Adeyum Saleh Ahmed hajafunga bao la pili. Sudan ilipata bao lake la kufutia machozi katika dakika ya 73 likiwekwa kimiani na Fabiano Elius Lako.
Aidha mechi nyingine iliyochezwa jana ilikuwa ni kati ya Ethiopia na Kenya ambapo timu hizo zilitoka suluhu. Kwa upande wa Bara, Kilimanjaro Stars, leo itakuwa kwenye uwanja wa Machakos ikicheza na timu mwalikwa Zambia.
Kilimanjaro Stars ina matarajio makubwa ya kushinda mechi hiyo inayotabiriwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana uimara wa Zambia. Mechi nyingine itakayochezwa leo ni kati ya Burundi na Somalia.
TIMU ya soka ya Taifa ya Zanzibar, ‘Zanzibar Heroes’ jana ilianza vema michuano ya Kombe la Chalenji baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Sudan Kusini.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Nyayo, Nairobi kuanzia saa nane mchana, timu zote zilionekana kushambuliana kwa zamu, lakini Zanzibar ilionekana kutumia uzoefu kuizidi maarifa timu ngeni kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Sudan Kusini.
Zanzibar ilikuwa ya kwanza kupata bao la kuongoza likifungwa na Suleiman Kassim Selembe kabla Adeyum Saleh Ahmed hajafunga bao la pili. Sudan ilipata bao lake la kufutia machozi katika dakika ya 73 likiwekwa kimiani na Fabiano Elius Lako.
Aidha mechi nyingine iliyochezwa jana ilikuwa ni kati ya Ethiopia na Kenya ambapo timu hizo zilitoka suluhu. Kwa upande wa Bara, Kilimanjaro Stars, leo itakuwa kwenye uwanja wa Machakos ikicheza na timu mwalikwa Zambia.
Kilimanjaro Stars ina matarajio makubwa ya kushinda mechi hiyo inayotabiriwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana uimara wa Zambia. Mechi nyingine itakayochezwa leo ni kati ya Burundi na Somalia.
Chanzo;Habari Leo


0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa