Home » » BANDA LA TCAA LAWAKUNA WENGI

BANDA LA TCAA LAWAKUNA WENGI

Banda la TCAAMAMIA ya wakazi wa maeneo mbalimbali ya Zanzibar wamefurika katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kujipatia elimu kuhusiana na masuala ya anga nchini.
Akizungumza na Tanzania Daima wiki iliyopita  katika viwanja vya Beit el tras  wakati ya maonesho ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Ofisa habari wa mamlaka hiyo, Ally Changwila,  alisema wakazi wa Zanzibar  wamekuwa wakijitokeza wakiwemo vijana ambao wengi wao walikuwa na hamu ya kujua namna ya wao kuwa marubani.
Changwila alizitaja sifa za mtu kuwa rubani ni awe angalau na ufaulu mzuri katika masomo ya Hesabu na Jiografia, awe na ufahamu mzuri wa lugha ya Kiingereza, afya njema, na awe amesoma kozi ya urubani.
Pia alisema pia awe amefanya mitihani maalumu inayotolewa na TCAA na kupatiwa leseni ya urubani.
Alisema kuna hatua mbalimbali za kusomea kozi za urubani. Zipo hatua za awali ambazo mafunzo yake yanatolewa hata hapa nchini ambayo mhitimu akimaliza anakuwa na uwezo wa kurusha ndege binafsi, na hatua nyingine ni ile ya marubani wenye uwezo wa kurusha ndege za abiria ambayo masomo yake yanatolewa  nje ya nchi ikiwemo Afrika Kusini.
Alisema kitendo cha baadhi ya wakazi hao kuonyesha nia ya kutaka kuwa marubani ni kizuri, hasa ulizingatia kada hiyo inakua kwa kasi nchini na uhitaji wa marubani unaongezeka siku hadi siku.
Chanzo;Tanzania daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa