Home » » Kusainiwa kwa Mkataba wa Makubaliano (MoU) kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kampuni ya kimataifa ya utafiti na Uzalishaji wa gesi (Shell)

Kusainiwa kwa Mkataba wa Makubaliano (MoU) kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kampuni ya kimataifa ya utafiti na Uzalishaji wa gesi (Shell)


 Wawakilishi kutoka Kampuni ya  Shell International Exploration na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwa katika mkutano Hague Uholanzi
---
 Kufuatia kusainiwa kwa Mkataba wa Makubaliano (MoU) kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kampuni ya kimataifa ya utafiti na Uzalishaji wa gesi (Shell) tarehe 28 Agosti 2013, wawakilishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Shell walikutana huko The Hague, Uholanzi kwa ajili ya uzinduzi wa kamati ya utekelezaji (JIC) tarehe 19 na 20 Januari 2014.Wakati wa mkutano huo, majadiliano muhimu yalifanyika katika maeneo ya kujenga uwezo, uwekezaji wa jamii na maendeleo katika mafuta na sekta ya gesi.

JIC ilianzishwa kwa lengo la utekelezaji wa makubaliano. Makubaliano yameainisha ushirikiano kati ya Shell na Zanzibar katika mafuta na sekta ya gesi na inaelezea shughuli za awali.

"Tunategemea ushirikiano wa muda mrefu na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya maendeleo ya sekta za mafuta na gesi Zanzibar," alisema Axel Knospe, mwakilishi Shell visiwani Zanzibar. "

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa