Zanzibar. Mamlaka ya Kodi ya Mapato Tanzania(TRA)Kanda ya
Zanzibar, imesema shehena ya magendo ya magogo yaliyoingizwa Zanzibar
kutokea Madagascar yatapigwa mnada au kuharibiwa baada ya Madagascar
kutoa ruhusa maalum imeeelezwa jana.
Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja wa
Operesheni wa TRA, Ali Bakari amesema kwamba kikosi kazi maalum cha
Taifa cha kupambana na vitendo vya ujangili wa misitu na wanyamapori
kimefika Zanzibar kufuatilia suala hilo.
Bakari alisema kikosi kazi hicho tayari kimetupa
barua pepe nchini Madagascar kuwataarifu kuhusu kukamatwa kwa mzigo huo
na kuwataka kutoa maelezo yakinifu iwapo mzigo huo ulitoka nchini humo
na hatua zipi zichululiwe ikiwemo kupigwa mnada au kuharibiwa.
Alisema kwa mujibu wa sheria ya Utawala wa Forodha
ya mwaka 2004, Kamishna wa TRA amepewa uwezo wa kutaifisha mzigo wa
magendo ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za kuupiga mnada na
kuutaifisha.
“Tunasubiri majibu ya baruapepe toka nchini
Madagascar, hapa kwetu ipo sheria inayotupa uwezo aidha kuupiga mnada
mzigo huo, kuuharibu au kuutaifisha kwa mujibu wa sheria,” alisema
Bakari.
Alisema kikosi kazi hicho ndicho kilichopokea
taarifa ya kuwepo kwa biashara ya magendo ya magogo toka Shirikisho la
la Forodha Duniani (WCO) katika kukabiliana na ujangili wa ukataji wa
miti adimu katika orodha ya hifadhi ya misitu ya dunia na kufanikiwa
kuukamata mzigo huo Zanzibar.
Aidha Bakari alisema iwapo mzigo huo utapigwa
mnada, sehemu ya fedha zake zitatumika kulipia gharama katika Bandari ya
Zanzibar ambako mzigo huo umekaa kwa kipindi husika chini ya uangalizi
wa bandari.
Msimamo huo wa TRA umetolewa siku moja baada ya
Wizara ya Kilimo na Maliasili Zanzibar kueleza kuwa mzigo huo
utarudishwa Madagascar.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment