Home » » UVCCM YAMTETEA IDD,WAMSHAMBULIA MAALIM SEIF

UVCCM YAMTETEA IDD,WAMSHAMBULIA MAALIM SEIF

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Makamu wa Kwanza wa Raisi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
 
Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), imesema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, hana mpango wowote wa siri wa  kuisambaratisha Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).

Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka,  alisema ikiwa serikali ya SUK itavunjia wakati wowote,mwanasiasa anyestahili kubebeshwa lawama  ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif  Sharif hamad, kwa kuwa ndiye anaeidhoofisha SUK kutokana na matendo yake.

“Makamu wa Kwanza wa RaIsi  Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ndiye anayeiyumbisha Zanzibar na  ikiwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa  itavunjika  asitafutwe mchawi, ”alisema Shaka katika mkutano wa hadhara. Alisema siri za Serikali zinavuja zimekuwa vikivuja na kujulikana katika makao makuu ya CUF kutokana na Maalim Seif kutokuwa mwaminifu.

Shaka alisema pamoja na kuundwa SUK, lakini bado Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais  Zanzibar anasahau mtafaruku wa kisiasa uliokuwapo Zanzibar  kabla ya maridhiano.

Akizungumzia msimamo wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutaka kuwasilisa hoja binafsi katika kikao kijacho na wananchi kuulizwa  kupitia kura ya maoni kama wanaafiki SUK iendelee au la, Shaka alisema hoja binafsi hupelekwa na mwakilishi baada ya kuijengea nguvu ya hoja na si ya chama cha siasa  hivyo anayetaka kufanya hivyo ana haki isiyozuilika.

Alisema hata hoja iliyopendekeza SUK haikuwasilishwa barazani na  CUF au CCM bali ilipelekwa  na mwakilishi wa Mgogoni, Aboubakary Khamis Bakary wa CUF kama  Mwakilishi Salmin Awadh Salmin wa CCM  jimbo la Magomeni  atakavyoipeleka kwenye chombo hicho ikisubiri maamuzi  kupitia kura ya maoni.

Maalim seif alipotafutwa jana kuzungumaia madai hayo hakupatikana.
 
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa