Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais wa Muungano na
Mazingira Mh. Luhaga Mpina wa Pili kutoka Kushoto akimuelezea Balozi
Seif Mikakati ya Ofisi yake kuwajibika Zaidi Zanzibar katika dhana nzima
wa kuimarisha Muungano wa Tanzania.
Picha na – OMPR – ZNZ.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema kwamba Serikali zote
mbili ile ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar zitaendelea kujenga mazingira mazuri ya uwezeshaji katika
kuhakikisha lengo lililokusudiwa na Taifa la kupatikana kwa Katiba Mpya
ya Tanzania linafanikiwa vyema.
Alisema
jukumu la kuratibu kazi ya kupatikana kwa Katiba hiyo kupitia kura ya
Maoni itakayopigwa na Wananchi baada ya kumalizika kwa Bunge Maalum la
Katiba itakuwa chini ya usimamizi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania
{ NEC } na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar { ZEC }.
Balozi
Seif Ali Iddi alitoa kauli hiyo wakati wa mazungumzo yake na Uongozi wa
Ofisi ya Makamu wa Rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
ukiongozwa na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira Mh. Luhaga Mpina yaliyofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini
Zanzibar.
Alisema
Wananchi walio wengi Bara na Zanzibar bado wanaamini kwamba Tanzania
inahitaji kuendelea kuongozwa na Serikali zinazozingatia haki ,usawa na
Utawala bora na hili litapatikana zaidi iwapo Katiba Mpya itayokidhi
vigezo hivyo itakamilika kwa mujibu wa Taratibu baada ya kupigiwa kura
na Wananchi wenyewe.
Balozi
Seif alieleza kwamba wakati Taifa linaelekea kujiandaa na mipango hiyo
Serikali zote mbili zitakuwa tayari kupambana na kikundi au mtu ye yote
atakayeonyesha dalili za kutaka kutishia amani ya Taifa iliyopo hivi
sasa.
Alimueleza
Naibu Waziri huyo wa Ofisi ya Makamu wa Rais wa Muungano na Mazingira
na Ujumbe wake kwamba vyombo vya dola kwa pande zote mbili havitasita
kuwashughulikia wale wote watakaoamua kutaka kuichezea amani ya Nchi.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliishukuru Serikali ya Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa ukaribu wake wa ushirikiano na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar uliopelekea kustawisha maendeleo ya Wananchi wa
pande zote mbili.
Alifahamisha
kwamba Watanzania wote ni wamoja. Hivyo kuna kila sababu ya kuendelea
kuimarisha Muungano uliopo wa pande hizo mbili ulioasisiwa na Marehemu
Mzee Abeid Aman Karume na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere Aprili 26 Mwaka 1964.
“
Historia itaendelea kubakia ikionyesha kwamba Wananchi wa Tanzania na
Bara na wale wa Zanzibar ni wamoja kutokana na muingiliano wa kidamu
uliopo kabla ya hata ya kuja kwa Muungano uliopo sasa ”. Alisema Balozi
Seif.
Akizungumzia
Taasisi za Serikali ya Muungano zilizoamua kutaka kujenga majengo yake
ya Kudumu Visiwani Zanzibar kwa lengo la Kuimarisha Muungano Balozi Seif
alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iko tayari kuzipatia maeneo
ya ujenzi Taasisi hizo.
Alisema
zipo Taasisi ikiwemo Ofisi ya Makamu wa Rais wa Serikali ya Jamuhuri ya
Muungano pamoja na Kituo cha utafiti cha Taifa { COSTEC } tayari
zimeshapatiwa maeneo na zimeshajenga Ofisi zao hapa Zanzibar.
Mapema
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga
Mpina aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea
kusimamia amani kabla na baada ya uchaguzi Mkuu.
Mh.
Luhaga alisema rasilmali nyingi zilizopo nchini ambazo zinaendelea
kufaidisha maisha ya Wananchi walio wengi bado zinasimama juu ya amani
inayoendelea kusimamiwa na Serikali.
Katika
kuimarisha Muungano Naibu Waziri Luhaga Mpina alimueleza Balozi Seif
kwamba tayari ameshamuagiza Katibu Mkuu Wake kufanya utaratibu wa
kumpatia Nyumba ya Kudumu Zanzibar ili kumpa fursa ya kutekeleza
majukumu yake kwa uhakika.
Alisema
tabia ya kukodiwa hoteli kwa ajili ya makaazi yake anapokuwa Zanzibar
kwa shughuli za kikazi ikiwa ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania ni vyema itaachwa mara moja.
Mh.
Luhaga alieleza kwamba yeye ni mshirika wa mazingira jambo ambalo
anawajibika kufanya kazi akiwa karibu na Waziri mwenzake anayesimamia
mazingira kwa upande wa Zanzibar.
Akikabidhi
Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi { NEC }kuhusu uchaguzi wa Rais,
Wabunge na Madiwani wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mnamo Tarehe 23
Juni 2016 Ikulu Mjini Dar es salaam Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji
Mstaafu Daniel Lubuva alisema Tume hizo zimepewa jukumu la kushughulikia
kura ya Maoni.
Jaji
Lubuva alisema kilichopo kwa sasa kwa watendaji wa Tume hizo ni
kuangalia changamoto zilizomo ndani ya sheria ya kura ya Maoni nambari
11 ya mwaka 2013 kwa ajili ya kuandaa mswaada wa marekebisho
utakaopelekwa Bungeni hapo baadae.
Mwenyekiti
huyo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania aliwathibitishia Watanzania
katika Mkutano huo kwamba kura ya Maoni itapigwa kama Katiba
ilivyofafanua licha ya mabadiliko ya ratiba yake kuchelewa kutokana na
kuingiliana na Uchaguzi Mkuu.
0 comments:
Post a Comment