Home » » WAZIRI WA AFYA ATEMBELEA UJENZI WA VITUO VIPYA VYA AFYA VINAVYOJENGWA KWA USHIRIKIANO WA SERIKALI YA ZANZIBAR NA UHOLANZI KUPITIA MRADI WA ORIO

WAZIRI WA AFYA ATEMBELEA UJENZI WA VITUO VIPYA VYA AFYA VINAVYOJENGWA KWA USHIRIKIANO WA SERIKALI YA ZANZIBAR NA UHOLANZI KUPITIA MRADI WA ORIO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Rans Nassor Salim Khamis inayojenga vituo 15 vya afya vya Mradi wa Orio alipotembelea kituo cha Kiboje wa pili (kulia) Meneja Ujenzi wa Kampuni ya Rans Ali Nassor.
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akitembelea ujenzi wa kituo kipya cha afya Kiboje akiambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kati Mashavu Sukwa (kushoto) meneja wa Ujenzi wa Kampuni ya Rans Ali Nassor.
Meneja wa Ujenzi wa Kampuni ya Rans Ali Nassor akimpa maelezo Waziri wa Afya juu ya ukarabati wa kituo cha afya cha Uroa alipofanya ziara ya kutembelea vituo vya Mradi wa Orio.
Muonekano wa kituo kipya cha afya cha Kijini Matemwe kinachojengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Uholanzi kupitia Mradi wa Orio.
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kijini Matemwe baadaya kuangalia maendelea ya ujenzi wa kituo kipya cha afya cha kijiji hicho.

Na Ramadhani Ali – Maelezo 

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendeleza dhamira yake ya kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya afya kwa kuimaisha huduma za afya na kujenga vituo vyenye hadhi vijijini.Dhamira hiyo inaendelea kutekelezwa kwa pamoja na wafadhili wa maendeleo wanaunga mkono juhudi zinazochukuliwa na Serikali katika kufikiaq malengo hayo.

Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo ameeleza hayo alipotembelea vituo vitatu vipya vya afya vya Kiboje, Kijini Matemwe na Chaani kubwa na kituo cha Uroa kinachofanyiwa ukarabati mkubwa.Amesema serikali ya Uholanzi kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia mradi wa Orio hivi sasa unaendelea na ujenzi wa vituo 15 vya afya nane vikiwa vinajengwa Unguja.

Waziri Mahmoud aliwaeleza wananachi wa sehemu hizo kuwa lengo la kujengwa vituo hivyo nikuwasogezea huduma za afya karibu na sehemu wanazoishi na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali kuu za mijin.Amewahakikishia wananchi kuwa vituo vinavyojengwa kupitia mradi wa Urio vitakapomalizika vitakuwa na vifaa vya kisasa na vitatoa huduma zote muhimu zikiwemo wodi za kujifungulia.

Aliongeza kuwa Wizaara ya Afya inajiandaa kuhakikisha kuwa vituo vyote vinavyojengwa vinakuwa na wafanyakazi wa fani zote muhiumu ili kuwapunguzia shida.“Wananchi wa Kijini kituo chenu ambacho ni cha daraja la pili kitakapomalizika kitatoa huduma zote muhimu na wagonjwa watatoka mjini kuja kutafuta matibabu hapa,”Waziri aliwahakikishia.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa