Home » » WANANCHI WAVUTIWA NA HUDUMA KATIKA BANDA LA MAONYESHO LA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA) ZANZIBAR

WANANCHI WAVUTIWA NA HUDUMA KATIKA BANDA LA MAONYESHO LA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA) ZANZIBAR

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
  Afisa Uhamiaji Ndg. Ali S. Nasor Mkuu wa Utawala na Fedha (DCI) Makao Makuu ya Ofisi ya Uhamiji ZanzIbar akiweka saini kwenye kitabu cha wageni alipotembelea banda la maonyesho la Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA) viwanja vya Maisara -  Unguja.
Wananchi waliotembelea Banda la Maonesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakifuatilia Vitambulisho vyao kutoka Shehia mbali mbali za Mjini Unguja, wakati zoezi la Ugawaji Vitambulisho likiendelea. 

Mamia ya wananchi wa Tanzania Zanzibar wameendelea kufurika katika viwanja vya Maisara Zanzibar kunakofanyika Tamasha la Nne la Maonyesho ya Biashara la Zanzibar; yakiwa ni sehemuu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi Zanzibar.

Katika maonyesho hayo pamoja na mambo Mengine Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa inatoa huduma ya ugawaji Vitambulisho vya Taifa, kusajiliwa kwa wale ambao hawakuwahi kusajiliwa pamoja na kupatiwa maelezo yanayohusu huduma zinazotolewa na Mamlaka.

Miongoni mwa Shehia ambazo Vitambulisho vinatolewa ni Mkunazini, Kiponda, Shangani,Kikwajuni juu, Kikwajuni Bondeni,Kisima Majongoo,Kiswandui, Malindi, Mchangani,Mwembe Tanga, Kilimani, Urusi, na Jang’ombe,.

Akizungummzia huduma zinazotolewa kwenye Banda hilo Meneja wa Mifumo wa Komputa ndugu Abdallah Mmanga amesema Wananchi waliofika kwenye Banda la NIDA kusajiliwa wanatakiwa kufika na nakala ya Cheti cha kuzaliwa, Vyeti  vya shule kuanzia na  Cheti cha kuhitimu Elimu ya Msingi, Pasi ya kusafiria (Pasport),Kadi ya Kupigia kura, Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, Leseni ya Udereva, Kadi ya Bima ya Afya, Kadi ya mfuko wa Jamii (NSSF,ZSSF,PPF,GEPF nk)

Pindi maonyesho hayo yatakapomalizika; wananchi ambao watakosa fursa wameshauriwa kufika kwenye ofisi za NIDA zilizopo kwenye kila Wilaya kwa Unguja na Pemba; ili kusajiliwa pamoja na kuendelea kuchukua Vitambulisho vyao kwa wale ambao wamekamilisha taratibu za Usajili.

Kwasasa Zanzibar imekamilisha Usajili wananchi Vitambulisho vya Taifa kwa asilimia 99 na mipango ya kuanza rasmi kwa matumizi ya Vitambulisho vya Taifa inaendelea kupitia wadau mbalimbali ili wananchi kuanza kunufaika.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa