Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kikosi cha Timu ya JKU kilichotwaa ngao ya Hisani
Kikosi cha Miembeni City
Ngao ya hisani
Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
TIMU ya JKU
imefanikiwa kutwaa taji la Ngao ya Jamii kuashiria ufunguzi wa msimu
mpya wa 2017-2018 wa Ligi Kuu ya Soka visiwani Zanzibar baada ya ushindi
wa wa mabao 2-0 dhidi ya Miembeni city katika Uwanja wa Amaan jioni ya
leo.
Mabao ya JKU yamefungwa na Salum Mussa dakika ya 47 na Nassor Mattar dakika ya 48.
Baada ya mchezo huo, maana yake pazia la Ligi Kuu ya Soka visiwani Zanzibar ndiyo limefunguliwa rasmi na ligi hiyo itaanza rasmi Oktoba 3, 2017 ambapo mechi za awali zitakua kama ifuatavyo.
3/10/2017
Mafunzo Vs JKU saa 8:00 mchana
J/Boys Vs KMKM saa 10:00 jioni
4/10/2017
Kilimani City Vs Kipanga saa 8:00 mchana
Charawe Vs KVZ saa 10:00 jioni
5/10/2017
Zimamoto Vs Taifa J saa 8:00 mchana
Polisi Vs Miembeni C saa 10:00 jioni
6/10/2017
Chuoni Vs Black S saa 10:00 jioni
Baada ya mzunguko huo ligi itasimama hadi tarehe 15/10/201
0 comments:
Post a Comment