Home » » UVCCM:AMANI YA EA NI JUKUMU LA PAMOJA

UVCCM:AMANI YA EA NI JUKUMU LA PAMOJA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
UVCCM: Amani ya EA ni jukumu la pamojaJUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), imesema kuwa kuchomoza kwa vitendo vya uhalifu katika ukanda wa Afrika Mashariki (EA) sanjari na matukio ya milipuko ya mabomu yaliyoleta maafa katika miji ya Mombasa, Arusha na Zanzibar ni jambo linalohitaji tahadhari ya pamoja ya vyombo vya ulinzi na usalama vya kikanda.
Kauli hiyo ilitolewa jana katika mkutano wa hadhara wa jumuiya hiyo uliofanyika kwenye viwanja vya Binti Amran mjini Unguja.
Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka, alisema kimsingi hivi sasa vyombo vya ulinzi na usalama vinatakiwa kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano na umakini mkubwa ili kuvitokomeza vitendo hivyo mara moja.
Aliviomba vikosi hivyo kujenga umakini na ushirikiano wa karibu katika kipindi hiki kigumu kuliko wakati wowote ili kufanya kazi kwa pamoja na kuibaini mitandao ya kihalifu katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki.
Hata hivyo, alizitaka Serikali mbili za Muungano na Zanzibar kuwakabili na kuwaasa viongozi wanaochanganya dini na siasa na kueleza kuwa jambo hilo likiachiwa linaweza kuzaa matatizo yatakayoleta madhara makubwa.
Alitolea mfano mataifa ya Syria, Nigeria, Somalia, Iraq, Misri na Jamhuri ya Afrika ya Kati kama yanayotatizwa hivi sasa kutokana na watu wake kutaabika, kupoteza maisha, huku watoto na wanawake wakihangaika.
Alisema kitendo cha kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar si tiketi itakayomsaidia Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kushinda urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa