Home » » TPB, ZSSF WAWABEBA WASTAAFU ZANZIBAR

TPB, ZSSF WAWABEBA WASTAAFU ZANZIBAR

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali IddMAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, amesema mpango wa utoaji mikopo kwa wastaafu ulioanza kutekelezwa, una lengo la kuwasaidia katika kukidhi mahitaji yao mbalimbali ya kimaisha.
Balozi Seif, alieleza hayo wakati akiuzindua rasmi mpango maalumu ulioandaliwa kwa pamoja kati ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), na Benki ya Posta Tanzania (TPB), wa ukopeshaji uliolenga kwa wafanyakazi wastaafu wa ZSSF, hafla iliyofanyika ukumbi wa hoteli ya Ocean View, Kilimani mjini hapa.
Mikopo hiyo inayotolewa na TPB kupitia Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, huwasaidia wastaafu kulipia gharama za matibabu, ada za shule kwa familia zao sambamba na kuendesha biashara ndogo ndogo zitakazosaidia kupunguza ukali wa maisha ya kila siku.
Balozi Seif alibainisha kuwa azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kujenga mazingira mazuri kwa wastaafu wake, ili kustaafu kwao kusiogopwe na kuonekana ni mwanzo wa kuanza kwa kipindi cha maisha ya shida yasiyokuwa na matumaini.
Alisema serikali inataka kuona wafanyakazi wake wanapopata barua za kustaafu, wasianze kuhuzunika kama ilivyozoeleka, kwa vile wengi kati yao huhisi kwamba wamefika wakati ambao hawawezi kukopesheka tena kutokana na udogo wa mapato yao wanayopewa kupitia pensheni zao.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa TPB, Sabasaba Moshingi, alisema kwa muda mrefu sasa taasisi mbalimbali za fedha hapa nchini zimekuwa hazitoi mikopo kwa wastaafu kwa dhana kwamba hawana uwezo wa kuirudisha.
Moshingi alisema Benki ya Posta kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar, ililiona tatizo hilo baada ya kutambua mchango mkubwa uliotolewa na wastaafu hao wakati wa utumishi wao na kufikia uamuzi wa kubuni mpango huo ambao ni mkombozi kwa wastaafu hao.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZSSF, Khamis Filfil Thani, alisema mafao ya wastaafu muda mwingi huongeza mapato ya taasisi za fedha na kuleta utulivu kwa wastaafu.
Alieleza kwamba mzunguko wa mafao ya wastaafu katika taasisi mbalimbali za kifedha  nchini, umefikia sh trilioni 2 wakati ule unaosimamiwa na ZSSF uliohusisha wastaafu 4,000 umefikia sh bilioni 20.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa