Home » » Walimu 70 wa sayansi kuajiriwa Zanzibar

Walimu 70 wa sayansi kuajiriwa Zanzibar

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali imesema ipo katika mchakato wa kuajiri jumla ya walimu wapya 70 wa masomo ya sayansi ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuondosha tatizo la uhaba wa walimu wa kada hiyo.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Mmanga Mjengo Mjawiri, alisema hayo wakati akitoa ufafanuzi kuhusu juhudi zinazochukuliwa katika kulipatia ufumbuzi tatizo la uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi.
Alizitaja juhudi zilizochukuliwa katika hatua ya awali ni pamoja na wizara kuwasiliana na Kamisheni ya Utumishi Serikalini ambayo imetoa kibali cha kuajiri walimu wapya wa masomo ya sayansi.
“Tupo katika mchakato wa kuajiri walimu wa masomo ya sayansi ambapo kwa sasa tumepata kibali kutoka Tume ya Utumishi Serikalini kufanya kazi hiyo,” alisema.
Alisema katika hatua ya awali wataajiri walimu 900, lakini kwa sasa wamepewa kibali cha kuajiri walimu 70 wa masomo ya sayansi.
Alisema kwa sasa walimu hao wataajiriwa kwa ajili ya masomo ya sayansi ambapo wapo katika hatua za mwisho za kufanyiwa udahili kwa ajili ya kazi hiyo.
Mjawiri alisema kuajiriwa kwa walimu hao kwa kiasi kikubwa kutasaidia kupunguza tatizo la upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi wanaohitajika katika shule mbalimbali za Unguja na Pemba.
Alisema kuajiriwa kwa walimu hao kutakwenda sambamba na mikakati ya Wizara ya Elimu ya kuimarisha maabara ya masomo ya sayansi zinazojengwa katika shule za sekondari Unguja na Pemba.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi kiasi cha kulazimika kuomba msaada kupata walimu kutoka nchini Nigeria.
CHANZO GAZETI LAHABARI LEO
 

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa